Announcements

Posted On: Apr 30, 2024


MKUTANO KATI YA TBS NA WAZALISHAJI, WAINGIZAJI NA WASAMBAZAJI WA BIDHAA ZA VIPODOZI HAPA NCHINI TAREHE 3 MEI, 2024

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeandaa mkutano kati yake pamoja na wazalishaji, waingizaji na wasambazaji wa vipodozi hapa nchini kwa lengo la kukuza uelewa wa matakwa ya Viwango vya bidhaa hizo. Mkutano huo utafanyika siku ya Ijumaa tarehe 3 Mei, 2024 katika ofisi za TBS Makao Makuu, Ubungo Dar es Salaam kuanzia saa 3:00 Asubuhi mpaka saa 7:00 Mchana.

tangazo kikao cha wadau wa vipodozi